Kapingaz Blog


Tuesday, June 18, 2013

BREAKING NEWSS! MH. JOSEPH MBILINYI 'SUGU' APATA AJALI AKIELEKEA ARUSHA

Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi amepata ajali wakati akielekea Arusha maeneo ya Hanang'
Taarifa za awali zinasema gari lake limegongana uso na uso na basi la abiria.
 
Taarifa zaidi tutawapa baadae.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AWAJULIA HALI MAJERUHI WA BOMU LA ARUSHA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa picha ya X-Ray, ya mmoja kati ya majeruhi waliolazwa kwenye Hospitali ya Mount Meru, Joseph Anthony, mkazi wa Karoleni, baada ya kujeruhiwa katika mlipuko wa bomu lililotokea wiki iliyopita katika mkutano wa Chadema eneo la Soweto jijini Arusha. Imeelezwa kuwa hadi jana Juni 17, 2013, wakati makamu alipowatembelea majeruhi hao watu watatu waliliripotiwa kufariki dunia. Picha na OMR  2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na wananchi wa jijini Arusha waliokusanyika nje ya Hospitali ya Mount Meru jana, wakati Makamu alipokuwa na ziara ya kuwatembelea kuwajulia hali majeruhi wa mlipuko wa Bomu uliotokea wiki iliyopita katika mkutano wa Chadema jijini Arusha, ambapo jumla ya watu 70 walijeruhiwa na watatu walifariki dunia. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mwilongo. Picha na OMR 3 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, aliyelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Selian, mkoani Arusha baada ya kudaiwa kushambuliwa mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akiwa katika uchaguzi mdogo wa Udiwani wa Kata ya Makuyuni, Monduli. Awali Nasari alikaririwa akieleza kuwa anamaumivu ya mgongo baada ya kushambuliwa na vitu vigumu na vijana wa Kimasai. Kwa mujibu wa maelezo ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,  Dkt. Paul Kweka, anayemtibu Mbunge huyo, alimueleza Makamu wa Rais kuwa mbunge huyo, baada ya kupimwa na kupigwa picha za X-Ray, ameonekana kuwa hana tatizo lolote la kiafya. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, aliyelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Selian, mkoani Arusha baada ya kudaiwa kushambuliwa mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akiwa katika uchaguzi mdogo wa Udiwani wa Kata ya Makuyuni, Monduli. Awali Nasari alikaririwa akieleza kuwa anamaumivu ya mgongo baada ya kushambuliwa na vitu vigumu na vijana wa Kimasai. Kwa mujibu wa maelezo ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,  Dkt. Paul Kweka, anayemtibu Mbunge huyo, alimueleza Makamu wa Rais kuwa mbunge huyo, baada ya kupimwa na kupigwa picha za X-Ray, ameonekana kuwa hana tatizo lolote la kiafya. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali, mtoto aliyetambuliwa kwa jina moja la Fahad (7) aliyelazwa katika chumba cha watu mahututi Hospitali ya Rufaa Selian, baada ya kujeruhiwa na mlipuko wa bomu katika mkutano wa Chadema, mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Arusha. Makamu wa Rais, jana Juni 17, alifanya ziara ya kuwatembelea kuwajulia hali majeruhi wa mlipuko huo waliolazwa katika hospitali za Mount Meru, Selian na Mtakatifu Elizabeth. Picha na OMR 6 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali, Gabriel Kivuyo (52) aliyelazwa Hospitali ya Rufaa Selian, baada ya kujeruhiwa na mlipuko wa bomu katika mkutano wa Chadema, mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Arusha. Makamu wa Rais, jana Juni 17, alifanya ziara ya kuwatembelea kuwajulia hali majeruhi wa mlipuko huo waliolazwa katika hospitali za Mount Meru, Selian na Mtakatifu Elizabeth. Picha na OMR 79 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Majengo A, Sarah John (45) aliyelazwa Hospitali ya Mtakatifu Elizabeth, baada ya kujeruhiwa na mlipuko wa bomu katika mkutano wa Chadema, mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Arusha. Makamu wa Rais, jana Juni 17, alifanya ziara ya kuwatembelea kuwajulia hali majeruhi wa mlipuko huo waliolazwa katika hospitali za Mount Meru, Selian na Mtakatifu Elizabeth. Picha na OMR

BALIMI YAENDELEA KUDHAMINI MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI MKOANI TABORA


Mgeni rasmi katika mashindano ya ngoma za asili kwa Mkoa wa Tabora Mstahiki Meya wa manispaa ya Tabora Gulamhussein Remtullah akizungumza na wakazi wa Mkoa huo katika mashindano hayo chini ya udhamini wa kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake ya Balimi Extra , mashindano hayo yamefanyika katika shule ya sekondari Iyungi.tolle
 Kushoto meneja wa matukio wa kampuni ya Bia Tanzania - tbl kanda ya ziwa  Bwana Erick Mwayela akimkabidhi Meya wa Manispaa ya Tabora Mstahiki Meya Gulamhussein Remtullah kitita cha shilingi laki sita ikiwa ni zawadi ya mshindi wa kwanza wa mashindano ya Ngoma za asili kwa mkoa wa Tabora mashindano hayo yamedhaminiwa na kampuni ya Bia Tanzania kupitia Bia yake ya Balimi Extra kulia aliyevaa fulani ya balimi ni kiongozi wa kundi la Mwenge la manispaa hiyo ambao ndio wameibuka washindi wa shindano hilo.
Meya wa Manispaa ya Tabora katikati Akimkabidhi kiongozi wa kundi la Mwenge fedha tasilimu shilingi laki sita mara baada ya kundi hilo kutangazwa Washindi wa shindano la ngoma za asili kwa mkoa wa Tabora ambalo limefadhiriwa na kampuni ya Bia Tanzania Tbl kupitia Bia yake ya Balimi Extra kulia kwake ni Meneja matukio wa kampuni hiyo kanda ya Ziwa Bw Eric Mwayela.

HATIMAYE FAINALI ZA MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI KWA MKOA WA TABORA AMBAYO YAMEDHAMINIWA NA KAMPUNI YA BIA TANZANIA-TBL KUPITIA BIA YAKE YA BALIMI EXTRA YAMEMALIZIKA RASMI KWA KUNDI LA MWENGE KUIBUKA BINGWA WA MASHINDANO HAYO NA KUJINYAKULIA KITITA CHA SHILINGI LAKI 6 NA HIVYO KUPATA TIKETI YA KUUWAKILISHA MKOA HUO KATIKA MASHINDANO YA KANDA YATAKAYO FANYIKA JIJINI MWANZA HIVI KARIBUNI.

KATIKA KINYANG'ANYILO HICHO AMBACHO KIMEVUTA HISIA ZA WAKAZI WENGI WA MKOA HUO, KUNDI HILO LIMEIBUKA MSHINDI KWA ALAMA 90 LIKIFUATIWA NA KUNDI LA MAGEREZA AMBAYO IMEPATA ALAMA 87 NA KUONDOKA NA ZAWADI YA SHILINGI LAKI 5 HUKU NAFASI YA TATU IKICHUKULIWA NA MASANGE JKT AMBAO WAMEJINYAKULIA SHILINGI LAKI 400 KWA KUPATA ALAMA 77, NAFASI YA 4 IMECHUKULIWA NA KUNDI LA MWAMKO SIKONGE NA KUJIPATIA SHILINGI LAKI 3KWA KUPATA ALAMA 63.

KATIKA MPAMBANO HUO AMBAO UMEVISHIRIKISHA VIKUNDI 10 WASHIRIKI WOTE KUANZIA NAFASI YA 5 MPAKA YA 10 WAMEJINYAKULIA ZAWADI YA FEDHA TASILIMU SHILINGI LAKI MOJA NA NUSU HUKU MEYA WA MANISPAA HIYO MSTAHIKI MEYA GULAMHUSSEIN REMTULLAH AMBAYE NDIYE ALIYE KUWA MGENI RASMI AKIIPONGEZA KAMPUNI HIYO KWA KUDHAMINI MASHINDANO HAYO AMBAPO KUPITIA MASHINDANO HAYO JAMII IMEKUWA IKIJIKUMBUSHA TAMADUNI ZETU.

GULAMHUSSEIN AMESEMA KUTOKANA NA KAMPUNI HIYO KUFANYA MASHINDANO HAYO KATIKA KIPINDI HIKI CHA MAVUNO HII INADHIRISHA KWAMBA BIA HIYO YA BALIMI EXTRA INAMJALI NA KUMSAMINI MKULIMA WA KITANZANIA.

AIDHA MEYA HUYO AMELITAKA KUNDU HILO LA MWENGE KWENDA KUUWAKILISHA VYEMA MKOA WA TABORA NA KUHAKIKISHA KUWA WANALEJEA NA USHINDI KATIKA MASHINDANO YA KANDA AMBAYO YANATALAJIA KUFANYIKA JIJINI MWANZA HIVI KARIBUNI.

AWALI MENEJA WA MATUKIO WA KANDA YA ZIWA BWANA ERICK MWAYELA AMESEMA KUWA KAMPUNI YAKE KUPITIA BIA YA BALIMI EXTRA WANAJISIKIA FAHARI KUDHAMINI MASHINDANO HAYO AMBAPO AMEFAFANUA KUWA KUPITIA MASHINDANO HAYO WATU WAMEKUWA WAKIFAHAMIANA NA KUKUMBUKA NGOMA ZA ASILI ZA MAKABILA YETU.

MASHINDANO MENGINE KAMA HAYO YANATALAJIWA KUFANYIKA MJINI SHINYANGA MWISHONI MWA WIKI IJAYO AMBAPO VIKUNDI MBALIMBALI VYA MKOA HUWA VITAPATA FULSA YA KUSHIRIKI KATIKA MPAMBANO HUO NA HIVYO KUWATAKA WAKAZI WA MKOA HUO KUJITOKEZA KWA WINGI ILI KUSHUHUDIA MWAKILISHI WAO KATIKA MASHINDANO YA KANDA.

Monday, June 17, 2013

MH. FREEMAN MBOWE AWATEMBELEA MAJERUHI NA WAFIWA WA BOMU LILILOLIPUKA SOWETO JIJINI ARUSHA


DSC09341Mwenyekiti wa Chadema, Mh freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Godbless Lema wakiwa katika uwanja wa Soweto, wakati wa zoezi la kuchukua vipimo mbalimbali chini ya usimamizi wa wataalamu toka Jeshini.
DSC09327
Mhe.Mbowe na Mhe. Lema wakishauriana jambo..
DSC09343Eneo la maafa. Inaelezwa kuwa wataalamu wa jeshi waligundua kuwako kwa kitu ndani ya tanki la mafuta na hivyo kuamua kulikata. Taarifa hizo zinadai kwamba kulikuwa na mabomu yametegwa chini ya gari na hivyo tank hilo lilishamabuliwa kwa risasi labda utokee mlipuko! Pia gari la matangazo lina majeraha mawili katika mlango wa kushoto yaliyotokana na kitu chenye ncha ambacho kinaweza kuwa risasi au vipande vya vyuma vya bomu.
DSC07458
Gari ambalo linasadikiwa kutegwa bomu katika tanki la Mafuta.

DSC09360Mh. Mbowe akiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao.
DSC09382James Ole Millya na Mbunge Lema wakimjulia hali mmoja wa majeruhi walilazwa katika hospitali ya Seliani Jijini, Arusha.
DSC09373Mtoto Sharifa nae amelazwa hospitalini hapo kwa majeraha ya mlipuko katika hospitali ya Seliani Jijini, Arusha.
DSC09377Dereva wa mgombea wa Chadema Kata ya Themi, Bw beni akiwa majeruhi kitandani,katika hospitali ya Seliani Jijini, Arusha.Habari hii kwa hisani ya Wazalendo 25 Blog

CCM YASHINDA KATA 16 KATI YA 22 UCHAGUZI WA MADIWANI



Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi, Nape Moses Nnauye.


Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22)  kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.
Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.
 Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka. Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.

Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.
 CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu. Tunawapa pole wale wote walioathirika na tukio hilo. Ni vizuri serikali ikalichunguza swala hili kwa kutumia muda mfupi na kuhakikisha waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua zinazostahili.

Pamoja na kulaani na kuitaka serikali kukomesha vitendo hivi nchini, ni wakati muafaka kwa vyama vya siasa nchini kujitazama upya kwani kuna kila dalili kuwa tukio hili kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari mhe. Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni la kupangwa, inawezekana limepangwa na Chadema wenyewe.
Hali ya kisiasa jijini Arusha kuelekea uchaguzi huo ilikuwa wazi kuwa wana Arusha walishaamua kuzirudisha kata hizo nne kwa CCM, hasa baada ya kuchoshwa na maandamano na vurugu za kila siku jijini Arusha. Aidha kauli za kukata tamaa za viongozi wa Chadema na vitendo vyao ni dalili tosha kuwa tukio hili lilipangwa na Chadema wenyewe.
CCM tunaendelea kusisitiza na kulaani juhudi za wenzetu kujaribu kujenga umaarufu wa chama chao juu ya damu za Watanzania. Juhudi hizi zinapaswa kulaaniwa na wazalendo wote ndani na nje ya nchi. Tukumbuke asiyekubali kushindwa, si mshindani. Si busara wala uungwana na ni kinyume na utu kutumia majanga ya kutengeneza kama mtaji wa kisiasa.
Lakini CCM tunalaani pia kitendo cha viongozi wa Chadema kujaribu kutumia baadhi ya misiba na majeruhi wa tukio hili kisiasa na mwisho wa siku kwenda kuwatelekeza hospitali baadhi yao baada ya kuwaahidi kubeba gharama zote za matibabu na mazishi.Tunaipongeza serikali kwa kuingilia kati na kuwasaidia waathirika hawa na kuhakikisha wanapata huduma inayostahili.
CCM inarudia kueleza masikitiko yake kwa waathirika wa tukio hili la kinyama na kikatili lisilostahili kuvumiliwa hata kidogo. Kama Chama tumeguswa sana na tukio hili pamoja na kulilaani, tunawasihi watanzania tushindane na kutofautiana bila kupigana na kuvunja tunu ya nchi yetu ya amani na utulivu. Katika demokrasia ya vyama vingi swala la kuvumiliana ni swala la msingi sana katika kufikia ukomavu wa demokrasia hiyo.
 
Imetolewa;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi.
17/06/2013

BOSS WA MALAWI CARGO TAWI LA MBEYA AFIKISHWA MAHAKAMANI AKITUHUMIWA KUJIHUSISHA NA RUSHWA YA NGONO

 

Bosi Mmalawi Evance Mwale akiongozwa na askari polisi kuingia katika chumba cha mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya ya Mbeya alikoshitakiwa kwa kosa la Rushwa ya Ngono na Ushawishi wa ngono, amerudishwa rumande baada ya kushindwa masharti ya dhamana.


Askari Polisi wakimrejesha rumande Bosi Mmalawi Evance Mwale anayeshitakiwa kwa makosa ya Rushwa ya Ngono
ALIYEKUWA  Meneja wa Kampuni ya Malawi Cargo tawi la Mbeya Evason Mwale(49) raia wa nchi jirani ya Malawi, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mbeya akituhumiwa kujihusisha na Rushwa ya Ngono.
 
Mwendesha mashtaka wa Serikali Basilius Namkambe akisoma Mashtaka ya mtuhumiwa huyo mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama hiyo Gilbert Ndeuluo alisema Mtuhumiwa anashtakiwa kwa makosa mawili ambayo ni Rushwa ya Ngono kinyume cha kifungu cha 25 cha Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa namba 11 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2007.
  
Namkambe alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa anashtakiwa kwa kosa lingine la matumizi mabaya ya madaraka kinyume cha kifungu cha 31 cha Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa namba 11 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2007.
  
Alisema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo April 11, Mwaka huu katika Hoteli ya Moja One Lodge iliyopo Iyunga Jijini Mbeya ambapo alikamatwa akitaka kujihusisha na rushwa ya Ngono na Mke wa Mfanyakazi wake.
 
Kwa upande wake Hakimu Mkazi Ndeoruo aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 1, Mwaka huu kwa ajili ya kuanza kusikiliza ambapo pia alisema Dhama iko wazi kwa Mtuhumiwa kuwa na wadhamini wawili wenye hati za mali isiyohamishika yenye thamani ya Shilingi Milioni 10, Barua zinazotambuliwa na mamlaka, ambapo pia mtuhumiwa  anatakiwa kuacha hati zake za kusafiria na kutoruhusiwa kutoka nje ya Jiji la Mbeya bila ruhusa ya mahakama.
 
Awali  ilidaiwa kuwa Meneja huyo alitaka kujihusisha na Rushwa na Mke wa Mfanyakazi wake wa nyumbani ambaye alimfukuza kazi na baadaye alimtumia Mkewe ili amrudishe kazini baada ya kufanya naye mapenzi.
Na Mbeya yetu

GERALD HANDO WA CLOUDS FM NUSURA AFUMULIWE NA BASTOLA LEO

 

 
MTANGAZAJI maarufu wa Clouds FM, Gerald Hando leo alfajiri alizua kizaazaa na kupelekea kutishiwa bastola na mtu ambaye jina lake halikufahamika mara moja.
Chanzo cha Saluti5 kimesema Hando aligonga gari la mtu huyo maeneo ya Kwa Kopa, jambo lililopelekea mtu huyo ashuke kwenye gari lake bastola ikiwa mkononi na kutishia kumfumua Hando.
Kama mtu huyo alidhani kutoa bastola ndio suluhisho basi alikosea sana, Gerald Hando anayetangaza kipindi cha "Power Breakfast" naye alishuka kwenye gari lake na kufungua shati lake na kuanza kumuamrisha mtu huyo afyatue bastola.
Huku akiporomosha matusi kwa ukali Hando alisema: “Piga hiyo bastola yako, shoot me.”
Hando aliendelea kuwa mkali huku akipigapiga kifua chake hali iliyovuta watu wengi kwenye tukio hilo ambao waliwasihi wote wawili kutuliza mzuka na kumfanya mtu huyo aliyekuwa na gari aina ya Rav 4 arudishe bastola yake kwenye gari na kutafuta njia nyingine ya kulimaliza tatizo lililotokea

KONYAGI YAWAPA SOMO WABUNGE KUHUSU BIASHARA YA KINYWAJI CHA VIROBA

Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa (kushoto) akifafanua jambo katika semina ya wajumbe wa Kamati mbili za Bunge za Uchumi,Viwanda na Biashara  pamoja na Kilimo,Maji na Mifugo kuhusu baadhi ya vyombo vya habari vyenye uhusiano na nchi jirani vinavyotumika kupiga vita viwanda vya ndani kikiwemo cha Konyagi. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa, akionesha kinywaji cha Afrika Kusini kilichofungwa kwenye viroba kama ambavyo Konyagi inafanya hapa nchini.Vinywaji kama hivyo vipo karibu nchi nyingi Ulimwenguni

Kwa picha zaidi bofya: HAPA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Czech kujiuzulu.

20136162151882734_4
 Waziri Mkuu  wa  Jamhuri  ya  Czec  Petr  Necas, ametangaza  kuwa   atajiuzulu  wadhfahuo hii leo.
Necas amekuwa akishinikizwa ajiuzulu  tangu  pale  Mnadhimu  Mkuu  wa  serikali Jana Nagyova, aliposhitakiwa  kwa rushwa  na  matumizi  mabaya ya  madaraka.
Wabunge  wawili  wa zamani akiwemo Waziri  wa  zamani  na  mkuu  wa  sasa  wa upelelezi  katika  jeshi  pamoja  na  mwenzake  wa  zamani pia  wamekamatwa. 
Rais Milos Zeman amesema  kuwa mashtaka  yao yamefunguliwa  baada  ya  polisi  kupekua  ofisi  za  serikali pamoja  na  za  binafsi  wiki  iliyopita.
Muungano  wa vyama  vinavyounda  serikali  ya  Necas  utajaribu  kuunda serikali  mpya, ambapo Kiongozi  atateuliwa  na  chama  chake  cha Civic Democratic.

Athman Bawji Mbwana ashinda Udiwani kata ya mianzini


 Mara baada ya matokeo kutangazwa na tume kupitia kwa Afisa Mtendaji wa Kata, Wanachama wa CCM waliletewa matokeo yale na kusomwa na Mkurugenzi wa uchaguzi wao ambaye ni Katibu kata wa Mianzini wa CCM, Abdallah Kihuku mbele ya hadhara ya Wana CCM waliofurika katika ofisi za kata .  
 Mshindi mteule wa Udiwani wa Kata ya Mianzini, Athman Bawji Mbwana akiongea machache kwa Wana CCM mara baada ya kutawazwa kuwa mshindi. Bawji anaziba nafasi iliyokuwa wazi kufuatia kifo cha diwani wa kata hiyo.
 Mwenyekiti wa Mkoa wa CCM, Ramadhan Madabida akiwashukuru wana CCM kwa umoja na mapambano ya dhati yaliyopelekea ushindi wa CCM. Huu ndio uchaguzi wake wa kwanza tangu awe Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam na ni uchaguzi mdogo wa pekee wa udiwani kwa Mkoa wa  Dar Es salaam.
 Katibu wa Mkoa wa CCM, Abdillah Mihewa naye pia akitoa yake ya moyoni.
 Katibu wa Wilaya ya Temeke wa CCM, Ndg Robert Kihaka akiwashukuru Wana CCM kwa uvumilivu wao na jitihada zao zilizozaa matunda mema.Picha na Emmanuel Shilatu wa NDG SHILATU BLOG

Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Mianzini, Athman Bawji Mbwana ameibuka mshindi wa uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Mianzini uliofanyika jana kwa kupata kura 1283, huku Mgombea wa Cuf akipata kura 494, Chadema wakiambulia kura 315 na ADC walipata kura 26, NRA kura 9 na Mgombea wa NCCR Mageuzi akiambulia kura 1. Bawji amemzidi mshindi wa pili kwa zaidi ya nusu ya kura

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YATAKA KASORO ZA SERIKALI YA MUUNGANO ZIJADILIWE KATIKA MCHAKATO WA KATIBA MPYA

 Waziri waNchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais  Mohd Aboud Mohd kulia akibadilishana mawazo na Waziri wa Afya Juma Duni Haji nje ya Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi mbweni nje ya mji wa Zanzibar.
Muwakilishi wa Jimbo la Uzini Mohd Raza akisisitiza jambo kwa Naibu Waziri wa Thuwaiba Edington Kisasi wamwanzo kushoto na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haji Omar Kheir wa mwanzo kulia katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Mbweni nje ya mji wa Zanzibar.
Muwakilishi wa Jimbo La Mji Mkongwe Ismail Jussa Ladhu wakwanza kushoto wakibadilishana mawazo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala bora Haji Omar Kheir katikati na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar Othman Masoud Othman katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi mbweni nje ya mji wa Zanzibar.Picha na Yussuf Simai-Habari Maelezo-Zanzibar
----
Na Khadija Khamis – Maelezo Zanzibar 17/06/2013
 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeeleza kuwa  kasoro zinazojitokeza katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania zinapaswa kuingizwa na kujadiliwa  katika mchakato wa Katiba unaoendelea.

 Hayo yalielezwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Muhammed Aboud Muhammed  katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, wakati akijibu suala la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Saleh Nassour Juma  aliyetaka kujua vigenzo vya  uteuzi wa Waziri Mkuu unaofanywa na Rais na Zanzibar imetoa Mwaziri Wakuu wangapi tokea kuasisiwa Muungano.

 Alisema Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ambayo hadi sasa ndio inayotuongoza haikueleza vigezo vya uteuzi wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania bali imetoa mamlaka ya uteuzi huo kwa Rais, na tangu kuasisiwa kwa Muungano  hadi sasa Zanzibar imetoa  Waziri mkuu mmoja ambae ni Salim Ahmed Salim.

 Alifahamisha kuwa tangu kuasisiwa kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Zanzibar haijawahi kutoa Spika wala Naibu Spika isipokuwa imewahi kutoa Mwenyekiti wa Bunge Zubeir Ali Maulid katika kipindi cha mwaka 2005/2010.

 Hata hivyo Waziri Aboud alisema kuwa  nafasi bado ipo ya kuweza kueleza kero  zilizopo ambazo zinaonekana kwamba ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muuungano ya Tanzania.
 Alikiri kuwa ipo hati ya makubaliano na maridhiano ya kikatiba kwa nchi  zote mbili zilizokuwa huru na mamlaka yake kamili na pia si kweli kuwa Zanzibar haina wasomi .

 Waziri alieleza kuwa kero za Muungano bado zipo na ndio sababu moja wapo ya  kuanzisha mchakato wa katiba ili kuzitafutia ufumbuzi  kero hizo.

 Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamesema  kuwa wanavyojuwa  ni kua Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi moja kero zilizozopo zinafanywa kwa makusudi

IDADI YA VIFO VILIVYOTOKANA NA MLIPUKO WA BOMU KWENYE MKUTANO WA CHADEMA MJINI ARUSHA VYAONGEZEKA NAKUFIKIA WATATU

 Baadhi ya majeruhi wa mlipuko wa bomu lililotokea mwishoni mwa wiki mjini Arusha.
---- 
ARUSHA, Tanzania

IDADI ya watu waliokufa kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea mwishoni mwa wiki wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikiwa katika mkutano wa kampeni za udiwani katika Kata ya Soweto mjini Arusha imefikia watatu.

Akitoa taarifa hiyo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mlongo amesema kuwa idadi hiyo imeongezeka baada ya majeruhi mmoja kufariki wakati akipata matibabu na majeruhi wengine bado wanaendelea na matibabu.

Tukio hilo limetokea wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za udiwani mkoani Arusha.

Wakati idadi ya vifo ikiongezeka hali ya majeruhi wengine si nzuri na wamekimbizwa nchini Kenya kwa ajili ya kupata matibabu zaidi.


Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya MkuuSeraUratibu na BungeWilliam Lukuvi amesema kuwa mtu hatakayefanikisha kupatikana kwa aliyehusika na tukio hilo atapata zwadi ya sh. milioni 100.

Akizungumza Bungeni mjini Dodoma leo, Mh. Lukuvi amesema kuwa serikali itatoa zawadi ya sh. milioni 100 kwa mtu atakayefanikisha kupatikana kwa mtu aliyehusika katika mlipuko wa bomu katika Kata ya Soweto mjini Arusha ambapo mkutano wa hadhara wa kampeni za udiwani zilikuwa zikifanyika.

Soma Tamko Maalum Kutoka Cham Cha Mapinduzi(CCM) Kufwatilia Kulipuka Kwa Bomu Kwenye Mkutano wa Chadema Soweto Mjini Arusha Pamoja na Mambo Mengine Lawaasa Chadema Kunyoosheana Videole Wenyewe Kwa Wenyewe


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza  na waandishi wa habari jana mjini Dodoma.   
-----

Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22)  kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.

 Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.
 Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka. Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.
 
 Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.

 CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu. Tunawapa pole wale wote walioathirika na tukio hilo. Ni vizuri serikali ikalichunguza swala hili kwa kutumia muda mfupi na kuhakikisha waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua zinazostahili.
Pamoja na kulaani na kuitaka serikali kukomesha vitendo hivi nchini, ni wakati muafaka kwa vyama vya siasa nchini kujitazama upya kwani kuna kila dalili kuwa tukio hili kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari mhe. Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni la kupangwa, inawezekana limepangwa na Chadema wenyewe.
 

 Hali ya kisiasa jijini Arusha kuelekea uchaguzi huo ilikuwa wazi kuwa wana Arusha walishaamua kuzirudisha kata hizo nne kwa CCM, hasa baada ya kuchoshwa na maandamano na vurugu za kila siku jijini Arusha. Aidha kauli za kukata tamaa za viongozi wa Chadema na vitendo vyao ni dalili tosha kuwa tukio hili lilipangwa na Chadema wenyewe.
 CCM tunaendelea kusisitiza na kulaani juhudi za wenzetu kujaribu kujenga umaarufu wa chama chao juu ya damu za Watanzania. Juhudi hizi zinapaswa kulaaniwa na wazalendo wote ndani na nje ya nchi. Tukumbuke asiyekubali kushindwa, si mshindani. Si busara wala uungwana na ni kinyume na utu kutumia majanga ya kutengeneza kama mtaji wa kisiasa.
 
 Lakini CCM tunalaani pia kitendo cha viongozi wa Chadema kujaribu kutumia baadhi ya misiba na majeruhi wa tukio hili kisiasa na mwisho wa siku kwenda kuwatelekeza hospitali baadhi yao baada ya kuwaahidi kubeba gharama zote za matibabu na mazishi.Tunaipongeza serikali kwa kuingilia kati na kuwasaidia waathirika hawa na kuhakikisha wanapata huduma inayostahili.

 CCM inarudia kueleza masikitiko yake kwa waathirika wa tukio hili la kinyama na kikatili lisilostahili kuvumiliwa hata kidogo. Kama Chama tumeguswa sana na tukio hili pamoja na kulilaani, tunawasihi watanzania tushindane na kutofautiana bila kupigana na kuvunja tunu ya nchi yetu ya amani na utulivu. Katika demokrasia ya vyama vingi swala la kuvumiliana ni swala la msingi sana katika kufikia ukomavu wa demokrasia hiyo.


 Imetolewa;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi.
17/06/2013 
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary

From The State House:President Jakaya Kikwete meets the Chairman and FIRST advisory council Rt. Hon Lord Hurd of Westwell

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete meets with the Chairman and FIRST advisory council Rt. Hon Lord  Hurd of Westwell(right) in London this morning. Left is FIRST Chairman Mr. Rupert Goodman .FIRST is a multi-disciplinary International affairs organization founded in 1984 with the aim to enhance communication between leaders in industry, finance  and governance and to promote dialogue at the strategic level. President Kikwete is in London to attend the G8 open for Growth, Tax and Transparency event. Photo by Freddy Maro-State House

BENKI YA NMB YA ZINDUA CHAP CHAP AKAUNTI KWAAJILI YA WATANZANIA WASIO NA AKAUNTI


IMG_1473 (2) 
Ofisa mtendaji mkuu wa benki ya NMB Mark Wiessing akimshukuru mheshimiwa waziri wa fedha Dk William Mgimwa mara baada ya kuzindua akaunti ya NMB Chap chap .
…………………………………………………………………..
Benki ya NMB imeendelea kuwa kinara katika kubuni na kuboresha huduma mbali mbali za kibenki, ili kuwawezesha wateja wake kupata unafuu na urahisi wa upatikanaji wa huduma za kibenki nchini Tanzania. Katika kulizingatia hili mwishoni mwa wiki Benki ya NMB ilizindua akaunti ya Chap Chap ambayo kusudi kubwa ni kuwafikia wananchi wote kule waliko na kuwafungulia akaunti zao.Kikubwa zaidi ni kwamba mteja ataweza kufungua akaunti papo hapo na kupata kadi yake ya kutolea fedha  ndani ya dakika  kumi

  • Mambo muhimuzaidiambayomtejawa Chap Chapanawezakufaidikanayonipamojana:
  • Kuonasalio la akauntiyakopopoteulipo
  • Kuwekafedhanakutoafedhakwamawakalawa M- pesa
  • KutumafedhakwawasionaakauntimahalipopotenchinikwakutumiahudumayaPesaFasta
  • Kununuavochazamudawamaongezikutokakwenyemtandaowowotewasimu
  • Kuchukuafedhahadishillingi 1.000,000/= kutoka kwenye ATM
NMB MgimwaMheshimiwa waziri wa fedha Dk William Mgimwa akichukuliwa alama za vidole na Ofisa mauzo ya Nje NMB Abdul Kandoro mara baada ya uzinduzi rasmi wa NMB chap chap akaunti mwishoni mwa wiki mkoani Dodoma
IMG_1469 
Sehemu ya maofisa na wageni waalikwa kwenye uzinduzi huo

HII NDIO SAFARI YA MWISHO YA MWANAMUZIKI LANGA: AZIKWA MAKABURI YA KINONDONI

Mwili wa marehemu ukiwasili katika makaburi ya Kinondoni.
Jeneza lenye mwili wa Langa likiingizwa kaburini.
 
Kwa picha zaidi bofya: HAPA

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA KISIMA CHA CHINI YA ARDHI CHA MANGAPWANI UNGUJA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja na msimamizi wa Kisima cha Chini kwa Chini, Abdulwakir Zahro, wakati alipofika kutembelea na kujionea Kisima hicho cha Chini kwa Chini, kilichopo Mangapwani, Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja jana Juni 15, 2013. Kushoto ni Mlezi wa Tamasha la Asili la watu wa Mangapwani, Ali Hassan Mwinyi. Picha na OMR 04 
Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiingia shimoni wakati alipofika Mangapwani Kutembelea na kujionea Kisima cha Chini kwa Chini, kilichokuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi huko ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea. Picha na OMR 011 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka shimoni kuangalia Kisima cha chini kwa chini kilichopo Mangapwani, ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea. Picha na OMR
012 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka shimoni kuangalia Kisima cha chini kwa chini kilichopo Mangapwani, ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea. Picha na OMR

SOMA KAULI YA RAIS JAKAYA KIKWETE KUHUSU SHAMBULIO LA MLIPUKO WA BOMU KWENYE MKUTANO WA CHADEMA ARUSHA NA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WAWILI NA MAJERUHI KADHAA

Rais Jakaya Kikwete
--
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa mfadhaiko, mshituko na huzuni kubwa taarifa za shambulio la mlipuko lililotokea katika mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mjini Arusha jioni ya leo, Jumamosi, Juni 15, 2013, tukio ambalo limesababisha vifo vya watu wawili na majeruhi ya Watanzania kadhaa.

Aidha, Rais Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa jamaa na ndugu wa wafiwa wote na pia ametuma pole nyingi kwa majeruhi ambao wameumizwa na kujeruhiwa katika tukio hilo ovu na katili.


Vile vile, Rais Kikwete amewatumia salamu za pole viongozi wa CHADEMA kufuatia tukio hilo la woga mkubwa na pia kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua stahiki za kuchunguza kwa haraka, kubaini, kuwakamata na kuwafikisha mbele ya sheria wote waliohusika na tukio hilo, wawe watu wa ndani ya nchi ama nje ya nchi.

Katika salamu zake za rambirambi na za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Magesa Mulongo, Rais Kikwete amesema: “Nimepokea kwa mfadhaiko, mshituko na huzuni kubwa shambulio la mlipuko lililotokea katika mkutano wa CHADEMA mjini Arusha jioni ya leo, tukio ambalo limesababisha vifo na majeruhi ya Watanzania wenzetu.”

Amesema Rais Kikwete: “Nakutumia wewe Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Magesa Mulongo salamu zangu za rambirambi kufuatia vifo na pole nyingi kutokana na majeruhi katika tukio hilo na naomba kupitia kwako unifikishie salamu zangu za rambirambi kwa jamaa na ndugu wa wafiwa na pole nyingi sana kwa majeruhi.”

“Kadhalika naomba unifikishie salamu zangu za pole kwa viongozi na wanachama wa CHADEMA kutokana na tukio hilo. Naomba uwajulishe kuwa uchungu wao ni uchungu wetu sote na msiba wao  ni msiba wetu pia. Nataka wajue kuwa tupo pamoja nao katika kipindi hiki kigumu na cha majonzi na huzuni mkubwa,” amesema Mheshimiwa Rais Kikwete.

Rais Kikwete amemwambia Mkuu wa Mkoa wa Arusha: “Kadhalika, nimeviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua za haraka kuwasaka wahusika, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria. Aidha, nawataka viongozi wa Serikali ngazi ya kitaifa, Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Arusha mjini kuhakikisha kuwa majeruhi wote wanapata matibabu ya haraka na huduma za tibabu stahiki.”

Aidha, Rais Kikwete ametoa wito maalum kwa wananchi akisema: “Kwa wananchi wenzangu, Watanzania wenzangu, napenda kutoa wito wa kuviachia vyombo vya ulinzi na usalama kufanya kazi yao vizuri ili tuweze kuwabaini waovu waliofanya kitendo hiki.”

“ Natambua kuwa yatakuwepo maneno mengi na hisia mbali mbali zitakazojaribu kulielezea tukio hilio ovu na katili kwa njia mbali mbali. Nawasihi tujiepushe na kuchukua dhana na hisia zetu au maneno ya watu wengine kuwa ni ukweli wa tukio hili. Tujipe nafasi ya kutafakari vizuri na kufanya uamuzi ulio bora.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Mimi siamini kuwa Watanzania au wafuasi wa vyama vya siasa wanachukiana kiasi cha kufanyiana matendo ya unyama wa aina hii. Naamini kuwa hiki ni kitendo cha mtu ama watu wasioitakia mema nchi yetu, watu ambao wanatafuta kila sababu ya kupandikiza chuki miongoni mwa raia ama makundi ya raia, ili nchi yetu iingie kwenye machafuko makubwa.”

“Ndugu zangu, Watanzania wenzangu, naomba tuzinduke,  ili tusiwape nafasi watu hawa waovu ya kuweza kutimiza malengo yao ya kuvuruga amani na utulivu wa nchi yetu kwa kuleta mifarakano baina yetu. Mungu Ibariki Tanzania, Munfu Ibariki Afrika.”
 
 Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU,
DAR ES SALAAM